MASHADA INC

Wednesday, September 5, 2012

EXCLUSIVE; MBEYA ALL STARS WAMJIBU IZZO BUSINESS


Wanamziki mbalimbali jijini Mbeya wamekanusha vikali kauli ya IZZO B kuwa wame copy na kupaste nyimbo yao mpya inayoitwa Mbeya Nyumbani iliyoimbwa na wasanii mbali mbali wa jijini Mbeya. Izzo amekaliliwa na vyombo vya habari akisema hajui chochote nahahusiki na Mbeya all stars akimaanisha wamecopy na kupaste kwa watu wa Kigoma (KIGOMA ALL STARS).

Akizungumza na UJIOWANGU BLOGSPOT mmoja wa wasanii na viongozi wa Mbeya all Stars DOCTOR FAZZI amesema "Mbeya all stars haijaanza leo wala jana ni tangu mwaka jana 2011 na nyimbo kibao zinathibitisha kwani tangu harakati za Ant Virus zinaendelea Mbeya all Stars ilikuwepo hata IZZO anajua hilo labda kinacho muuma ni kutoshirikishwa au kupewa taarifa"

Kimsingi Mbeya all Stars ilianza Mwaka 2011, huu ni mwendelezo wa projects zao, kilicho washtua wengi ni jinsi wanavyoendelea kujizolea Umaarufu kutokana na track yao mpya MBEYA NYUMBANI inayosumbua katika chat za media mbali mbali hapa nchini.

HII NI STATUS YA DOCTOR FAZZI FACEBOOK

TAMKO LANGU KAMA VICE PRESIDENT WA MBEYA ALLSTARZ
KWA OUR BROTHER IZO B, KWANZA
NADHANI HATA MUHESHIWA MP SUGU AKIISIKIA KAULI YA
IZO B'' ATAMSHANGAA 7BU KTK SHOW ZA ANTI VIRUS ILE
YA CCM UWANJANI MBEYA ALL STARS TULIALIKWA NA
TUKA PERFORM LIVE,
PIA MKOLONI ATAMSHANGAA 7BU KTK SHOW YA ANTI VIRUS
PALE SOKOINE ALIKTUWEKA KTK LIST JAPO WALIOPAFOM WALIKUWA
NI ISANGA FAMILY
EZDENI the ROCKA ATAISHANGAA PIA KAULI YAKE 7B
MWANZONI MWA HUU MWAKA TULIPOTOA WIMBO WA
TUSAIDIE ALITUFANYIA INTERVIEW PIA WIMBO ALIUPA PROMO
YA KUTOSHA, PIA
DJ DIZO THE PRACTICAL SKILLZ NA MANSHETA PIA WANAMSHANGAA
7BU WAO NDIO WALIOINZISHA MBEYA ALL STARZ TANGU MWAKA JANA
Djfredy Herbet PIA ATASIKITISHWA NA KAULI YA IZO B 7BU MWAKA JANA
ALITUPA SHOW PALE MTENDA SUNSET SIKU YA UHURU
Producerlosso Losso Jr. AKIISIKIA KAULI YAKE ATALIA MNO MAANA NI KAMA
ALIYETUTOA HAPO SIJAMSEMA Zest Juma NA EFFECTOR AMBAO TULIFANYA NAO
NYIMBO 1 1 KAZITANGU MWAKA JANA
NAKUMBUKA NILIFAHAMIANA NA Stanslaus Lambat MWAKA JANA 7BU
YA MBEYA ALL STARZ
KAKA KATUKOSEA SANA YEYE HAZIJUI SHIDA ZINAZOTUPATA WADOGO ZAKE HUKU MBEYA BILA KUFANYA UCHUNGUZI ANATAKA KUTUPOTEZA KUTUPOTEZA
KWENYE RAMANI YA MUZIKI WATU WA MKOA ALIOZALIWA,,
ALICHOONGEA SIO KABISA!!! AREKEBISHE KAULI YAKE!!

Fuatilia maelezo ya wasanii na wadau mbali mbali kuhusu kauli ya IZZO B na maoni yao hapa chini

HII NI VIDEO YA MBEYA ALL STARS;

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...